Image
Image

MOHAMMED Faki, beki mpya wa Simba ametua Msimbazi.


MOHAMMED Faki, beki mpya wa Simba ametua Msimbazi na kutamka kauli  moja kuwa “Yanga safari hii haina chake.”
Beki huyo aliyesajiliwa kutoka JKT Ruvu, alisema kuwa amefurahi mno kumwaga wino Msimbazi juzi Jumatano usiku, lakini kubwa ambalo amepania kulifanya kwa kikosi hicho ni kuhakikisha inakata minyororo ya utumwa ya kushindwa kutwaa taji la Ligi Kuu Bara tangu msimu wa 2011/2012.
Faki ambaye jana Alhamisi mchana alirejea kwao Zanzibar kwa ajili ya mapumziko alisema: “Ninafuraha ya kuwa ndani ya Simba na nina malengo ya kuipa ubingwa msimu ujao.
“Nitahakikisha ninacheza kwa kujitoa na kupambana kuipa Simba heshima ya kutwaa ubingwa bila kupoteza mchezo wowote.
“Lakini pia ninajua kuwa Simba wana upinzani mkubwa na Yanga, hivyo ninajua heshima kubwa ya mchezaji kwenye hizo klabu huchangiwa na mchezo wa watani, hivyo nitahakikisha ninaendeleza rekodi bora walizonazo Simba kwa sasa za kuifunga Yanga muda wowote ule.
“Yanga kwa Simba si kitu, mimi nimekuja Simba kufanya kazi na moja ya kazi zangu Simba itakuwa ni kuwadhibiti Yanga, lakini pia timu zote zitakazocheza dhidi yetu.”
Faki ambaye anasifika kwa nguvu na akili ya uwanjani, aliongeza kuwa msimu uliopita akiwa JKT Ruvu alipata nafasi ya kucheza dhidi ya Yanga na kudai kuwa ni timu ya kawaida licha ya kwamba waliwafunga katika mechi zote mbili.
“Ninachokiona kwa Yanga ni uzoefu tu, lakini ni timu ya kawaida na kutua kwangu Msimbazi nikiwa na wakali wengine, nina hakika Yanga watataabika sana msimu ujao,” alitamba Faki.
 Mbali ya mchezaji huyo,  pia kiraka za zamani wa Azam, Samir Nuhu alisaini mkataba na Simba juzi usiku jijini Dar es Salaam.
Usajili wa wachezaji hao wawili unaimarisha zaidi Simba ambayo msimu uliopita iliyumba na kuambulia nafasi ya tatu. Wengine ambao wameshasaini Simba mpaka sasa ni Peter Mwalyanzi kutoka Mbeya City na Mussa Mgosi aliyekuwa Mtibwa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment