Namibia ilifuzu katika kundi
A baada ya kumaliza kundi hilo kwa wingi wa alama saba na kupata ushindi muhimu
jana usiku baada ya kuishinda Zimbabwe mabao 4 kwa 1.
Katika mchuano mwingine,
Mauritius iliwashinda Ushelisheli bao 1 kwa 0.
Namibia sasa itamenyana na
Zambia katika hatau hiyo ya robo fainali juma lijalo.
Leo ni michuano ya kumaliza
kundi la B, na mchuano muhimu leo ni katia ya Madagascar na Swaziland kwa
sababu ni timu moja tu ndio inayostahili kufuzu.
Timu hizo zote zina alama 6.
Atakayefuzu atacheza na Ghana
katika hatua ya nusu fainali.
Mchuano mwingine ni kati ya
Tanzania na Lesotho zote ambazo zimeondolewa katika michuano hiyo kwa matokeo
mabaya.
0 comments:
Post a Comment