Image
Image

News Alert:Viongozi na watumishi wa Serikali wametakiwa kuwasaidia wakulima nchini ili wafikie malengo.


Viongozi na watumishi wa Serikali wametakiwa kuwasaidia wakulima nchini ili wafikie  malengo ya kuzalisha chakula pamoja na mazao ya biashara kwa lengo la kusaidia ukuaji wa sekta hiyo na pato la wakulima waliojiajiri katika sekta hiyo inayotajwa kuajiri zaidi ya asilimia sabini ya wananchi wote .

Rai hiyo imetolewa Mjini Iringa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe , Dakta REHEMA NCHIMBI  alipokuwa   akifungua kikao cha viongozi wa Serikali,Maafisa Kilimo pamoja na wafanyabiashara waliowekeza kwenye viwanda vya usindikaji mazao ya kilimo pamoja na maziwa .

Amsesema iwapo  Serikali itawasimamia vizuri wakulima na kuhakikisha wanapata pembejeo na masoko ya mazao yao kilimo , kuna uwezekano wa   kubadili maisha ya wakulima wadogo na kuwaondoa kwenye umaskini wa kipato .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa SAGCOT Centre ,Bwana GEOFREY KIRENGA amesema SAGCOT imekuwa kiunganishi kati ya wakulima,Serikali na taasisi zinazo ji shughuli sh a na biashara ya mazao ya kilimo pamoja na pembejeo kwa lengo la kuinua sekta ya kilimo na wakulima wenyewe .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment