Image
Image

Tanzania itakavyofaidi soko la vito vya thamani.


Tanzania imebahatika kuwa na aina nyingi ya madini ya vito vya thamani kama vile dhahabu, almasi na Tanzanite.
Wingi wa rasilimali hizo za thamani duniani umekuwa ukiwafanya baadhi ya watu kuamini kuwa nchi ni tajiri lakini unapoingia kwenye uhalisia, utajiri huo haulisukumi taifa kumea vizuri kiuchumi.
Je, tatizo ni nini? Kuna mipango gani ya kukabiliana na hali hiyo? Haya ni maswali ambayo yamekuwa yakiulizwa na wengi na makala hii inakusudia kuyajibu.
Arusha na moja ya mikoa nchini ambao kuna uchimbaji wa aina nyingi za madini. Moja ya madini yanayoupa sifa kubwa mkoa huu ni madini ya Tanzanite ambayo hayapatikani eneo jingine popote duniani.
Biashara kubwa ya madini hayo ipo katika Jiji la Arusha na kuna mitaa, ambayo ni kawaida kukuta vijana, wakiwa wamekaa kando ya barabara wakichonga madini na kuuza. Mitaa hiyo ipo katikati ya Jiji la Arusha kama vile Barabara ya Pangani, jengo la Chama cha Wafanyakazi Arusha (Ottu) na Mtaa wa St Thomas.
Katika mitaa hii, utakuta vijana wengi wakiwa na viti na meza ndogo wakichonga madini na wengine wakiuza. Mbali na Tanzanite, pia kuna aina nyingine madini kama vile saphire, spinel, tourmaline, sperssatite na aquamarine. Miongoni mwa madini hayo yapo yanayochimbwa mikoa ya jirani.
Kuuzwa holela kwa madini kunatajwa ndiyo kunasababisha madini mengi kutoroshwa na kuvuka mipaka kuingia nchi mbalimbali ambazo huziuza kwenye soko la dunia. Aina hii ya biashara hulikosesha taifa mapato na isitoshe hata wachimbaji na wafanyabiashara hiyo hapa nchini hupata faida kidogo tofauti na ingekuwa wangepeleka wenyewe kwenye soko la dunia.
Kwa mfano ripoti ya mwaka 2013 inaonyesha kuwa uuzaji wa madini ya Tanzanite uliingizia Tanzania Dola 38 tu za Marekani huku nchi zinazopata madini hayo kwa njia ya panya, zikijipatia mapato makubwa. Kulingana na ripoti hiyo, katika mwaka huo, Tanzanite iliingizia Kenya Dola 100 milioni na India Dola 300 milioni.
Tanzania yazinduka
Kwa kutambua namna inavyopoteza mapato na nchi kutofaidika kikamilifu na madini yake, Serikali imeamua kuweka mkakati ambao utaziba mianya ya utoroshaji wa madini nchini. Ili kuifanya biashara ya madini ya vito, kutambulika kisheria na kuinufaisha Serikali katika kukusanya kodi mipango imeanza kujengwa kituo cha kukata, kusanifu na kuuza madini Arusha.
Kituo hiki, kinakuwa cha kimataifa, ambacho kitakusanya wafanyabiashara wa madini ya Tanzanite wa ndani na nje ya nchi kukaa pamoja kufanya biashara halali.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene anasema kituo hiki, kitajengwa na Serikali kwa kushirikiana na Kituo cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment