Image
Image

Bidhaa zisizo na nembo ya TBS marufuku Sabasaba.

MAONESHO ya 39 ya Kimataifa ya Biashara yameanza rasmi jana huku kukipigwa marufuku kuingiza bidhaa zisizo na nembo za ubora au vifungashio bora.
Maonesho ya mwaka huu yatafunguliwa rasmi Ijumaa ijayo na Rais Jakaya Kikwete huku kukiwa na banda maalumu la masuala ya elimu kumwezesha kujua vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi na kupata wafadhili.
Siku hiyo ya jana baadhi ya washiriki waliendelea kupanga bidhaa zao katika mabanda huku wengine wakimalizia ukarabati wa mabanda.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE), Jacqueline Maleko alisema kuwa maonesho ya mwaka huu hawataki kuona bidhaa zisizo na nembo, bidhaa feki pamoja na vifungashio hafifu kama asali kuweka katika chupa za konyagi.
Maleko alisema pia wamepiga marufuku biashara ndogo barabarani hivyo wameandaa sehemu yenye meza kwa ajili ya biashara hizo. “Pia hatutaki mavuvuzela au vyombo vinavyotoa sauti ili kufanya kuwa maonesho ya biashara ya kuwezesha watu kupata oda na siyo kuuza,” alisisitiza.
Alisisitiza kuwa ulinzi umeimarishwa kwa sehemu zote kuwa na vifaa maalumu vya usalama ili kudhibiti wezi ma matukio mbalimbali. “Licha ya kuwa vifaa hivyo vilikuwepo tangu mwaka jana lakini tumeviongeza kwani mwaka jana tuliwakamata watu wawili kwa kutumia vifaa hivyo mmoja aliiba simu na mwingine aliwaibia laptop wafanyabiashara wa nje,” alisema.
Alisema nchi ambazo kampuni zimeongezeka ni pamoja na Japan ambayo ilikuwa na kampuni 10 lakini mwaka huu kuna kampuni 17, India, China, Italia, Pakistani nchi nyingine kufikia makampuni zaidi ya 400.
Akizungumzia kuchelewa kupangwa kwa bidhaa mpaka jana yalipoanza maonesho alisema mabanda mengi yaliyo wazi ni ya washiriki kutoka nje ambao wanashiriki siku chache.
Alisema kawaida maonesho ya kimataifa ni siku nne au tano lakini haya yanafanyika siku 10 hivyo wataanza kufika kuanzia Julai mosi mwaka huu huku wale wa ndani alisema wamejenga tabia ya kuchelewa tu.
Maonesho hayo yanashirikisha nchi 25, kampuni zaidi ya 400 kutoka nje ya nchi na 4,700 za nchini huku kukiwa na wizara sita.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment