Image
Image

Manji:Najisikia faraja kuiongoza Yanga.

MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji amesema anajisikia faraja kuwaongoza wanachama na mashabiki wa klabu hiyo, kwani imemfanya aishi maisha ya mani yeye na familia yake.
Kutokana na kitendo hicho Manji  ameahidi kuiongoza klabu hiyo vyema hadi hapo itakapofika mwisho wake.
Akizungumza Dar es Salaam jana na viongozi wa matawi mbalimbali ya klabu hiyo, Manji alisema anajisikia faraja kuwa na marafiki wengi kuliko maadui hivyo ana imani hata atakapostaafu ataendelea kuishi maisha ya upendo na amani.
Alisema anapata thawabu kuwaongoza wanachama na mashabiki wa Yanga, ambao hufurahia kila timu yao na hali hiyo imekuwa ikimpa furaha katika maisha yake.
Mwenyekiti huyo alisema amefanya mambo mengi mazuri ndani ya Yanga, tangu alipochaguliwa kwa mara ya kwanza akiwa kijana mwenye umri wa miaka 33.
"Kutokana na mambo mazuri niliyoyafanya wazee wa Yanga, walinichagua kuwa Chifu  wa kwanza katika klabu hii  jambo ambalo ninajivunia nikiwa kiongozi hadi nitakapostaafu uongozi wangu," alisema Manji.
Alisema anajivunia kuwa Mwenyekiti wa klabu hiyo kongwe nchini akiwa na miaka 36 hadi sasa na kwamba anashukuru kuona Yanga, mpaka leo inafanya vyema katika michuano mbalimbali.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment