Image
Image

Upinzani wazidi kuibana mbavu serikali tozo ya mafuta.

Kambi rasmi ya upinzani bungeni, imerudia ushauri wake kwa serikali wa kuitaka isipandishe tozo ya mafuta kuepuka mfumuko wa bei, huku ikiitaka kuzingatia ripoti ya Chenge ambayo ilianisha vyanzo vipya vya mapato.
Waziri Kivuli wa Fedha, James Mbatia (pichani), alisema kinachofanywa na serikali kuongeza kodi ni kuongeza ugumu wa maisha ya Watanzania hasa wa kipato cha chini. 

 "Tulipendekeza maeneo kadhaa ambayo pia yalipendekezwa na kamati ya Spika ya kuisaidia serikali kuibua vyanzo vipya vya mapato na kutoa taarifa yake kwako, maarufu kama Chenge 1, lakini kwa kiasi kikubwa serikali haijafanyia kazi ipasavyo taarifa hii," alisema. 

Alisema ni vema taarifa hiyo ikatekelezwa na mapato yatapatikana katika kuendeleza sekta ya umeme, maji, elimu, afya badala ya kubebesha mzigo huo kwa Watanzania.

 "Tunazidi kuitaka serikali iangalie na kutumia vyanzo vipya vya mapato hasa sekta ya uvuvi katika Bahari Kuu  ukusanyaji wa kodi za majengo kwa ufanisi, mazao ya misitu na kuweka utaratibu wa kurasimisha sekta isiyo rasmi katika tasnia mbalimbali za uchumi na kuongeza asilimia 40 ya Pato la Taifa,"alisema.

 Kwa mujibu wa Mbatia, mabadiliko katika sheria ya leseni za biashara inayoweka sharti kuwa ili mfanyabiashara aweze kupata leseni ya biashara lazima awe na hati ya ukaguzi wa kodi, iwapo itaanza kutumika Julai mosi, mwaka huu, italeta usumbufu mkubwa kwa wafanyabiashara pamoja na kujenga mianya ya rushwa, urasimu na migogoro baina ya wafanyabiashara na serikali.

 Alisema hakukua na ushirikishwaji wa wadau na kwamba hayajaandaliwa mazingira rafiki na yanayojitosheleza katika utekelezaji wa sheria na kwamba halmashauri zimejiwekea viwango visivyotabirika na vinavyobadilika mara kwa mara vya kodi ya leseni.

 Waziri huyo alisema miradi ya uwekezaji ya hadhi maalum ambayo itapewa misamaha mikubwa ya kodi kwa wenye masharti ya uwekezaji wa dola za Marekani, ni muhimu kwa serikali kutoa taarifa bungeni kuhusu utaratibu iliyojiwekea wa kutoa vivutio hivyo na ufanisi wa utekelezaji.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment