Image
Image

Wachezaji Mwadui wanusurika kifo.

WACHEZAJI wawili na makocha wawili wa timu ya Mwadui ya Shinyanga wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali mkoani Dodoma.
Wachezaji hao ni kiungo wa zamani na kipa wa zamani wa Yanga, Nizar Khalfan na Shaaban Kado. Kado, ambaye amejiunga na Mwadui akitokea Coastal Union, ameumia vibaya mkono wa kulia katika kiwiko.
Walipata ajali hiyo jana saa saba mchana eneo la Bahi mkoani Dodoma wakienda Shinyanga kuendelea na mazoezi waliyoanza jijini Dar es Salaam kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Agosti.
Makocha wao, kocha msaidizi Habib Kondo na yule wa makipa aliyetambuliwa kwa jina la Adam Khalid, wamepata michubuko. “Tunashukuru tuko salama, ajali hii ni mbaya, tungeweza hata kugonga basi lililokuwa mbele yetu,” alisema Khalid.
Katika basi hilo kulikuwa na wachezaji wengine takribani 10 wakiongozwa na Julius Mrope. Hata hivyo, gari lao aina ya Toyota Grandis limeharibika vibaya hasa nyuma baada ya kupasuka matairi ya kulia na kuchomoka.
Kado na Nizar waliondoka kwa basi la Isamilo Express kuendelea na safari wakiungana na wenzao waliopanda basi hilo kuanzia Dar es Salaam. Mwadui FC iliyopanda Ligi Kuu msimu ujao, inaanza maandalizi ya ligi inayoanza Agosti 22, mwaka huu.
Wengine ni Malika Ndeule, Said Sued, Jabir Aziz na wengineo. Gari hilo lilikuwa likiendeshwa na Kondo, beki wa zamani wa klabu kadhaa nchini.
Gari hilo lina namba za usajili T444 DCX. Wachezaji hao walipewa huduma ya kwanza eneo la ajali na kisha polisi kuandika maelezo yao.
Mwadui inafundishwa na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ambaye inaelezwa alitumia usafiri wa ndege jana kwenda Shinyanga. Akizungumza kwa njia ya simu jana, Kihwelo alikiri kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa Kado aliumia kidogo kiwiko cha mkono na waliruhusiwa kuondoka kuenda Shinyanga.
Alisema kuwa timu hiyo ilikuwa ikienda Shinyanga kuendelea na mazoezi yaliyoanza jijini Dar es Salaam wiki moja iliyopita.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment