Image
Image

Azam fc yakomaa,yatinga fainali kagame,inakutana na gor mahia.


Fainali ya Kombe la Kagame sasa itakuwa ni Azam FC dhidi ya Gor Mahia ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumapili.

Azam FC imekuwa ya pili kuingia fainali kwa kuitwanga KCCA kwa bao 1-0 huku Gor Mahia ikiwa imetangulia baada ya ushindi dhidi ya timu ngumu ya Al Khartoum.

Hii ni mara ya pili kwa Azam FC kuingia fainali ya Kagame, mara ya kwanza ikiwa ni 2012 ambapo ilifungwa na Yanga iliyokuwa ikifundishwa na Tom Saintfiet ambaye sasa ni kocha wa timu ya taifa ya Togo.

Mechi ya fainali itachezwa Jumapili, ikitanguliwa na ile ya mshindi wa tatu kati ya KCCA dhidi ya Al Khartoum.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment