Image
Image

LOWASSA ajiunga ukawa na kuibwaga CCM*Apokelewa kwa shangwe kama mfalme*Aweka bayana mbinu zilizotumika kukata jina lake Dodoma.



Pichani kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi Mh James Mbatia, Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe, Waziri mkuu mstaafu Mh Edward Lowassa na Mwenyekiti wa CUF Prf Ibrahimu Lipumba.

Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe akimkabidhi kadi ya kujiunga na CHADEMA Waziri mkuu mstaafu Mh Edward Lowassa.

Mh Freeman Mbowe akimkabidhi kadi ya Kujiunga na CHADEMA mama Regina Lowassa.
Waziri Mkuu mstaafu Mh Edward Lowassa na Mkewe mama Regina Lowassa wakionyesha kadi zao za Uanachama wa CHADEAMA mara baada ya kujiunga na CHADEMA katika hafla iliyofanyika Bahari Beach Hotel.
Waziri Mkuu mstaafu Mh Edward Lowassa akiwa na Mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahimu Lipumba
Mwenyekiti wa Baraza la wanawake CHADEMA na Mbunge wa Kawe Mh Halima Mdee akisikiliza kwa makini yaliyokuwa yakijili katika hafla ya kujiunga na Chadema kwa Waziri Mkuu Mstaafu Mh Edward Lowassa.

Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania Mheshimiwa EDWARD LOWASSA a mesema  ameamua kukihama Chama Cha Mapinduzi na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA,  baada ya kutafakari kwa  kina  yaliyotokea katika mchakato wa kumpata mgombea  urais kupitia Chama Cha Mapinduzi.
Mheshimiwa LOWASSA amesema hayo jijini Dar es salaam katika mkutano ulioandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kwa niaba ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi-UKAWA kumpokea kama wanachama mpya wa CHADEMA.
Amesema mchakato wa kuteua wagombea ulighubikwa na mizengwe , ukiukaji wa maadili, uvunjaji wa katiba na taratibu za uchaguzi ndani ya CCM.
Aidha,amesema uchaguzi ulisimamiwa kwa upendeleo na chuki iliyokithiri dhidi yake.
Amesema kikatiba ya Chama Cha Mapinduzi, Kamati ya maadili siyo chombo rasmi na haina madaraka ya kuchuja na kupendekeza majina miongoni mwawale wanaoomba kugombea urais kupitia CCM.
Amesema kilichotokea Dodoma ni kupora madaraka ya Kamati Kuu na kuikiuka katiba ya CCM.
Mheshimiwa LOWASSA Kamati Kuu ya Halmashauri kuu iliitishwa na kuburuzwa ili ielekeze azma ya watu binafsi pasipo kujali demokrasia, katiba. Kanuni na taratibu za uchaguzi ndani ya CCM.
Wakati huo huo idadi kubwa ya wanachama wa Chama ChaMapinduzi katika halmashauri ya Ushetu wilayani wamehamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kwa madai kuwa wamechukizwa na kile wanachokiita fitina zinazoendelea katika Chama Cha Mapinduzi.
Aidha, wamesema wamefanya hivyo kumuunga mkono mbunge wao JAMES LEMBELI katika harakati za ukombozi wa kweli kwa wananchi pamoja na wakulima wa tumbaku na pamba wanaodhulumiwa kila kukicha.
Matukio hayo yametokea kwa nyakati tofauti katika mikutano ya aliyekuwa mbunge wa Kahama kwa tiketi ya CCM Mheshimiwa JAMES LEMBELI ambaye amehamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo -CHADEMA
Katika hali isiyotarajiwa mke wa mwenyekiti wa halmashauri ya Ushetu  JUMANNE KIMISHA,  JUSTINE KIMISHA amechukua fomu ya kugombea udiwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo -CHADEMA pamoja na mumewe anayegombea kupitia Chama Cha Mapinduzi.
Amesema aliwekwa mizengwe na kuzushiwa majungu na uongo mwingi kuhakikisha kuwa jina lake halifikshwi mbele ya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu kujadiliwa, licha ya ukweli usiopingika kuwa alikuwa mgombea aliyeungwa mkono na wanachama na wananchi wengi zaidi kuliko wenzake wote.
Amesema kibaya zaidi ni kile kitendo cha kuwanyima wagombea 38 haki ya kujieleza mbele ya Kamati Kuu.
Amesema kwa kifupi anaamnini kuwa hakutendewa haki katika mchakato mzima wa kupendekeza majina na kuteua mgombea urais kupitia CCM.
Amesema baada ya kutafakari kwa kina ameamua kuwa kuanzia leo anaondoka CCM na kuitikia wito wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo -CHADEMA kuungana nao katika kuleta mabadiliko ya kweli kwa nchi.
Wakizungumza katika mkutano huo, viongozi wakuu wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi-UKAWA wamempongeza Mheshimiwa LOWASSA na kumuahidi kumpa ushirikiano katika azma yao ya kuwaletea wananchi maendeleo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment