Image
Image

Azam yakiri kupata upinzani Zanzibar.

NAHODHA wa timu ya Azam FC, Himid Mau amekiri kupata upinzani mkali katika mechi yao ya kirafiki na ya kumalizia ratiba ya mazoezi visiwani Zanzibar na JKU iliyochezwa juzi Amaan mjini hapa.
Mau alisema kuwa pamoja na timu yao kuibuka na ushindi, lakini wamepata wakati mgumu kuivaa ngome ya wapinzani wao hao ambao walijiandaa kwa kila idara. Mau aliyaeleza hayo juzi usiku mara baada ya kumaliza mchezo wao wa kirafiki na timu hiyo ambapo waliweza kushinda mabao 2-0.
Alisema kuwa timu ya JKU ni timu nzuri ambayo kama itaweza kupata mechi zaidi za kirafiki za kimataifa wanaweza kufanya vizuri katika michuano yao kimataifa watakayoshiriki.
“JKU ni timu nzuri ambayo ni mechi pekee ambayo tumeongeza kitu kati ya mechi zetu tatu tulizocheza, na sisi tumeshinda kutokana na udhoefu tu lakini JKU kiboko”, alisema.
Hata hivyo, alisema kuwa mchezo wao ulikuwa mzuri kwa kila upande na kuendelea kusifia kiwango kizuri kilichooneshwa na wapinzani wao hao ambao waliwafunga kwa udhoefu. Katika mchezo huo Azam ambayo ilitarajiwa kuondoka jana, mabao yake yalifungwa na John Boko dakika ya 65 na Abubukar Sure Boy dakika ya 85.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment