Image
Image

Mkwasa alia na Yanga, Azam FC.

KUSHINDWA kuwepo kambini kwa wachezaji wa Yanga na Azam FC kumeharibu ratiba ya maandalizi ya timu ya taifa, Taifa Stars, inayojiandaa kwa mchezo wa kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Nigeria.
Taifa Stars itaikaribisha Nigeria, Super Eagles katika mchezo wa kufuzu kwa fainali hizo zitakazofanyika Gabon 2017, huku Tanzania ikipangwa Kundi G pamoja na Nigeria, Misri na Chad.
Tayari Stars imeshafungwa 3-0 na Misri katika mchezo wa kwanza uliofanyika mjini Alexandria na kushika mkia katika kundi lake ikifuatiwa na Chad, ambayo nayo haina pointi lakini ilifungwa mabao 2-0 na Nigeria, ambayo ni machache ukilinganisha na Stars. Misri inayoongoza kundi hilo kwa kuwa na pointi tatu sawa na Nigeria, iko juu kwa kuwa na idadi kubwa ya mabao.
Akizungumza jana, Kocha Mkuu wa muda wa timu hiyo, Charles Mkwasa alisema ratiba yake ya maandalizi imetibuka baada ya wachezaji wa Yanga na Azam FC kuzuiwa kujiunga na timu hiyo.
Alisema wachezaji hao watajiunga na timu hiyo baada ya mchezo wa Ngao ya Jamii utakaozikutanisha timu hizo Jumamosi Agosti 22 kwenye Uwanja wa Taifa na kuondoka usiku kwenda Muscat, Oman, ambako Jumatatu watacheza mchezo wa kirafiki.
Mkwasa alisema wachezaji hao watafanya mazoezi siku moja tu, muda ambao hautoshi na yote hiyo imechangiwa na Yanga na Azam FC kutokuwa tayari kuwaachia wachezaji wake kwa ajili ya mechi ya Ngao ya Jamii.
Taifa Stars imepata mwaliko wa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Taifa ya Oman Agosti 24 usiku, ambapo baada ya mchezo huo timu hiyo itasafiri kwenda Uturuki jijini Istanbul.
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Oman (OFA) liliomba kuche za mchezo wa kirafiki na Taifa Stars kabla ya kuwavaa Turkemebistan katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia Septemba 03 kwa bara la Asia, ambapo kocha wake mkuu Mfaransa Paul Leguen aliomba kucheza na Stars.
Mara baada ya mchezo huo, Taifa Stars itakwenda Istanbul kwa kambi ya wiki moja, ikiwa nchini Uturuki, Stars inatarajiwa kucheza michezo miwili ya kirafiki kabla ya kurejea nchini kucheza na Nigeria Septemba 05.
Imeelezwa kuwa Mkwasa mwishoni mwa wiki atatangaza kikosi cha wachezaji 22 watakaosafiri kwenda Uturuki kwa kambi hiyo. Aidha, mshambuliaji Adi Yussuf anayechezea klabu ya Mansfield Towny ya Uingereza alitarajiwa kujiunga na Stars nchini Uturuki, hatajiunga tena kwa sababu ya maumivu.
Adi aliumia wiki iliyopita katika mchezo dhidi ya Nottingham Forest, ambapo kwa sasa anaendelea na matibabu chini ya uangalizi wa klabu hiyo, na pindi atapokuwa fit atapata nafasi ya kujumuika na kuitumika timu ya Taifa ya Tanzania.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment