Image
Image

Kaseja kujiunga na Klabu ya Mbeya City ya jijini Mbeya.

Aliyekuwa kipa wa mabingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, Yanga, Juma Kaseja, anakaribia kujiunga na Klabu ya Mbeya City ya jijini Mbeya.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana jijini, mazungumzo kati ya Kaseja na viongozi wa klabu hiyo yako katika hatua za mwisho na wakati wowote anaweza kusaini mkataba wa kujiunga na timu hiyo.

Taarifa zaidi zinaeleza kwamba, Mbeya City wameamua kufanya mazungumzo na Kaseja kutokana na kufahamu uzoefu wake kwenye ligi hiyo ambayo msimu ujao inatarajiwa kushirikisha timu 16 kutoka mikoa mbalimbali nchini.

Hata hivyo, maamuzi ya kumsajili nyota huyo, yanapingwa na baadhi ya mashabiki wa Mbeya City ambao ni wapenzi na wanachama wa Yanga.

Katibu Mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe, aliliambia gazeti hili jana saa 11:52 jioni kwamba bado hawajasaini mkataba lakini wako kwenye mazungumzo na kipa huyo ambaye aliwahi pia kuzidakia Simba, Moro United na timu ya Taifa (Taifa Stars).

Kaseja kwa sasa ni mchezaji huru lakini bado anakabiliwa na kesi ya madai iliyofunguliwa na Yanga ambao wanadai nyota huyo alikatisha mkataba huku pia kipa huyo akisema klabu hiyo ilivunja mkataba naye kwa kushindwa kumlipa sehemu ya pili ya malipo yake ya usajili ya Sh. milioni 20 kama walivyokubaliana kwenye mkataba.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment