Akizungumza
na maefu ya
wananchi katika uzinduzi huo
Mh.Lowasa ambaye amesema akichaguliwa kuwa
raisi atahakikisha sekta zote
ambazo zimezorota kutokana
na kukosa usimamizi
ikiwemo Elimu ,Kilimo ,na sekta ya
usafirishaji ukiwemo wa reli na Anga.
Kwa upande
wake mgombea mwenza Mh.Duni Haji amesema maelfu
ya wananchi na viongozi
wanaendelea kuunga mkono
mabadiliko ni ishara ya
kutosha kuonyesha kuwa
wamechoshwa na uonevu
na mabavu ya
serikali ya CCM.
Ukafika wakati wa viongozi
mbalimbali wa UKAWA wakiongozwa
na Mwenyekiti wa CHADEMA Mh.Fereeman
Mbowe ambao wamesema dalili ya kwanza ya
kuonyesha kuwa viongozi wa CCM hawathamini wananchi
ni kujifanya maskini huku
wakificha utajiri wao.
Baadhi
ya mawaziri waliokihama
chama cha mapinduzi
akiwemo Mh.Fredrik Sumaye
na Laurence Masha ambao
pamoja na kumpongeza Mh.Lowasa kwa kuongeza
mabadiliko wamesema waliyatamani siku
nyingi lakini alishindwa
kwa sababu ya mfumo
ulioandaliwa kwa makusudi
ya kuwatia hofu
na kuwatisha huku
wakielezea baadhi ya maovu yanayofanyika
chini ya serikali
ya CCM.
0 comments:
Post a Comment