Image
Image

Finland kukata mishahara ya mawaziri ili kupunguza matumizi serikalini.


Ofisi ya Waziri Mkuu nchini Finland imetangaza mpango wake wa kutaka kupunguza mishahara ya mawaziri kwa aslimia 5.
Serikali ya Finland ilichapisha mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2016 siku ya Jumatatu iliyoonesha kiwango cha fedha Euro bilioni 54.1 zinazotazamiwa kukidhi mahitaji ya nchi.
Finland inalenga kuhifadhi fedha Euro milioni 2 kila mwaka kwa kupunguza mishahara ya mawaziri kwa asilimia 5 kuanzia muhula mpya wa mwaka 2015-2019.
Vile vile, mawaziri wote watatakiwa kufanya kazi bila malipo kwa wiki moja kila mwaka.
Maelezo zaidi ya ofisi ya waziri mkuu yamearifu kwamba utaratibu huo mpya pia utawekewa makatibu wa wizara na wasaidizi wao.
Kwa sasa mawaziri wa Finland hupokea mshahara wa fedha Euro 9,788 huku waziri mkuu akilipwa Euro 11,742 kwa mwezi.
Hapo awali, waziri mkuu Juha Sipila aliwahi kupunguza idadi ya wizara kutoka 19 hadi 14 na ofisi za makatibu kutoka 9 hadi 4 kama mojawapo ya hatua za kupunguza matumizi ya fedha nchini serikalini.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment