Image
Image

Wanachi wazuia msafara wa LOWASSA kwa muda kumueleza kilio chao Muheza.

Msafara wa mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa umepata wakati mgumu hivi leo Muheza mkoani tanga baada ya wananchi kuzuia msafara wake kwa muda kutaka asimame waongee naye kabla ya kufika sehemu anayo elekea kuhutubia.
Mh.Lowassa ambaye alikuwa kwenye gari ya wazi aambalo anafanyia nalo mikutano yake huko jijini Tanga ililazimu kusimama kuwasikiliza huku gari hilo likiwa limezungukwa na wananchi hao ambao ni wapenda mabadiliko huku wakiimba nyimbo zenye imani na Mh.Lowassa na kuahidi kuwa hawata muangusha Octoba 25 kwakuwa wanapenda mabadiliko.
Jana vilevile Mkutano wa LOWASSA  katika jiji la Tanga ulikumbana na balaa la aina yake baada ya watu kadhaa kuzimia, huku wengine kujeruhiwa na kisha mabomu kadhaa ya machozi kuvurumishwa na polisi kutawanya maelfu ya wafuasi muda mfupi baada ya kumalizika.
Hali ya mkanganyiko katika mkutano huo wa Lowassa, anayeungwa mkono pia na muungano wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vya NLD, NCCR-Mageuzi na Chama cha Wananchi (CUF), ilianza kuonekana mapema wakati maelfu ya watu walipojitokeza kwenye viwanja vya Tangamano.
 Baadhi ya watu, hasa wanawake walijikuta wakiwa hoi hoi kutokana na joto na kukosa hewa, hali iliyowalazimu wahudumiwa Msalaba Mwekundu kuingilia kati na kutoa huduma ya kwanza kwani wengi wao walionekana wakizimia na kuanguka chini.
Hata hivyo leo hii huko muheza wananchi kwa nyakati tofauti wamekua wakisema kuwa wana imani ya asilimia 100 na Mh.LOWASSA kua akichaguliwa kuwa rais wa Tanzania kilio chao cha kutapa tapa bila ajira kitapatiwa ufumbuzi kwakuwa wanamuona ni mtu mwenye maamuzi magumu na mpenda mabadiliko.
Wananchi hao wamesema kuwa hawaoni sababu ya kila kukicha kilio kikubwa kwa vijana ni ajira jambo ambalo limekuwa nijanga la taifa miaka nenda rudi,hadi kusababisha vijana wengi kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya na mambo mengine,ambapo wamesema wanaendelea kusikiliza sera za kila mmoja wa wagombea lakini kwa mwaka huu lazima wafanye mabadiliko ili waone ahadi zitolewazo bila kutekelezeka je zitatekelezeka.
Baada ya muda nitakuletea ripoti kamili kutoka Muheza,Like Page yetu na kuwa wa kwanza kusoma taarifa zetu.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment