Image
Image

Kasi ya Rais Magufuli kutumbua majipu yawafurahisha AFP.

CHAMA cha siasa cha Alliance for Tanzania Farmers (AFP) kimetoa pongezi kwa Rais John Magufuli na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa kasi ya utendaji kazi ambayo wameionesha na kuleta matumaini kwa wananchi.
Wakizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, viongozi wa chama hicho walisema kasi aliyoanza nayo Dk Magufuli ndio kasi ambayo wananchi wengi walikuwa wakiitamani siku zote.
“Watanzania walio wengi wamefurahishwa sana na maamuzi mbalimbali ambayo Rais amekuwa akiyatoa hasa kufuta safari za nje pamoja na kufuta baadhi ya maadhimisho ambayo yalikuwa yakitumia fedha nyingi za umma huku wananchi wakiteseka,” alisema Mkurugenzi wa Mahusiano na Makundi Maalumu wa AFP, Peter Sarungi.
Sarungi alisema maamuzi ya Rais kufuta safari za nje zisizo na tija kwa taifa pamoja na matamasha na maadhimisho mbalimbali yataleta ufanisi kwa watendaji wa serikali na kuwafanya wananchi kuwa na matumaini mapya.
Alisema Dk Magufuli anaishi katika maneno yake ambayo alikuwa akiyazungumza kipindi cha kampeni na sasa anayafanyia kazi kwa vitendo jambo ambalo ni faraja kwa walio wengi.
“Watanzania tulio wengi tupo nyuma yake na huyu ndio aina ya kiongozi ambaye tulikuwa tunamtaka ili tufikie tunapotaka,” alisema Sarungi.
Aidha, Sarungi alisema mbali na kuwapongeza viongozi hao, lakini pia walimtaka Waziri Mkuu Majaliwa kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo chini ya ofisi yake.
Miongoni mwa mambo waliyotaka kufanyiwa kazi ni kuboresha na kuandaa mikakati mipya ya kuimarisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa kuiongezea makali ikabiliane na rushwa nchini.
Upande wa Rais, alisema akasimamie vyema afya za watu wenye ulemavu, wazee, wanawake na watoto zinaboreshwa kwa kiwango cha juu na kuhakikisha anakomesha mauaji ya albino na vikongwe.
Mbali na hayo, viongozi hao AFP chenye makao makuu yake visiwani Zanzibar, walisema Dk Magufuli ahakikishe Tanzania Bara na Zanzibar zinabaki na umoja wao kwa kudumisha Muungano.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment