Image
Image

Latest News:Kamati kuu ya CCM yapitisha jina la NDUGAI kuwania Uspika.



Kamati ya wabunge wote wa chama cha mapinduzi CCM kwa kauli moja wamepitisha jina la mbunge wa kongwa mkoani Dodoma Mh.Job Ndugai kugombea nafasi ya Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma Mapema Leo.

Kuteuliwa kwa jina la Ndugai ni baada wagombea wengine wawili kujitoa katika kinyang"anyiro hicho cha Uspika ndani ya chama cha CCM .

Waliojitoa katika mchakato huo wa kuchaguliwa katika nafasi ya Uspika ni pamoja na Mhe Abdullah Ali Mwinyi na Dr Tulia Ackson Mwansasu hivyo kupisha nafasi hiyo kwenda kwa Mh Job Ndugai.

Katibu wa itikadi na uenezi taifa Bwana Nape Nauye amesema kukamilika kwa uteuzi huo wa nafasi ya Uspika kunatoa nafasi kwa wabunge wote wa CCM kumfanyia kampeni Mh.Job Ndugai ili aweze kuchaguliwa na wabunge wote katika mkutano wa bunge la kumi na moja linalotarajiwa kuanza hapo kesho mjini Dodoma.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment