Image
Image

TRA imesema mpaka mwishoni mwa mwezi Oktoba ilikuwa imefikia asilimia 97.6 ya Malengo.


Mamlaka ya mapato -TRA imesema mpaka mwishoni mwa mwezi Oktoba  ilikuwa imefikia asilimia 97.6 ya malengo waliyokuwa wamewekewa na serikali  ya kukusanya kodi kwa mwaka huu  ambapo walikuwa wamekusanya  shilingi trilioni 12.3.

Kamishina mkuu wa mamlaka hiyo Rished Dade amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika miezi ya Novemba na Desemba wanatumai watakuwa wamekusanya kodi zaidi ya asilimia mia moja ya lengo walilokuwa wamekewa na serikali.

Kuhusiana na agizo la rais Dr.John Magufuli kuziba mianya ya ukwepaji kodi na kuwabaini wakwepa kodi ,kamishina Bade amesema mamlaka yake  itahakikisha inalitekeleza hilo na kuwa sasa imeendelea na mkakati wake wa kukutana na wadau mbalimbali wa masuala  ya kodi kuzungumza nao juu ya kulifanikisha hilo.

Nao moja kati ya wadau wakuu wa  ulipaji kodi nchini mawakala wa forodha-TAFFA  kupitia mwenyekiti wao Steven Ngatunga amesema  wapo tiyari wao na taasisi zingine za kibiashara nchini kushirikiana TRA katika kuibaini mianya ya ulipaji kodi ili kumuwezesha Dr.Magufuli na serikali ya awamu  ya tano kutimiza  malengo yake.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment