Image
Image

Urusi imeonya kuwa italipiza kisasi kufuatia kuangushwa kwa ndege yake.

Urusi imeonya kuwa italipiza kisasi kufuatia kuangushwa kwa ndege yake.
Waziri mkuu wa Urusi , Dmitriy Medvedev, amesema kuwa Uturuki inawalinda Islamic State .
Medvedev amedai kuwa Uturuki inahofia kupoteza kipato kikubwa inachofaidika kutokana na wizi wa mafuta kutoka Syria.
Aidha, Medvedev amedai kuwa mikataba yote na Uturuki imesimamishwa na kuwa kampuni zote zenye asili ya Uturuki zimepigwa marufuku nchini Urusi.
Hayo yamejiri huku rais wa Marekani Barack Obama amemhakakishia mwenzake rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan kuwa nchi yake inaiunga mkono Uturuki katika jitihada za kulinda mipaka yake.
Hakikisho hilo la rais Obama linafwatia hatua ya Uturuki kuidungua ndege ya Urusi karibu na mpaka wa Syria.
Mataifa yote duniani yalihofia kutibuka kwa vita iwapo Moscow ingelipiza kisasi kufuatia mauaji ya askari wake katika shambulizi hilo.
Ikulu ya WhiteHouse ilisema kuwa wakati wa mazungumzo kwa njia ya simu kati ya marais hao wawili kuwa wote walikubaliana kutuliza hali hiyo.
Umoja wa mataifa na muungano wa kujihami ya nchi za Maghraibu NATO wamewataka Urusi na Uturuki kutuliza hasira zao.
Akizungumza baada ya mkutano wa dharura wa mataifa ya NATO ulioitishwa na Uturuki, katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amesema tathmini ya tukio hilo inaonyesha kuwa ndege ya kivita ya Urusi iliruka katika anga ya Uturuki.
Huku kukiwa na hali ya wasiwasi, Stoltenberge ametaka kuwepo na hali ya utulivu kutoka pande zote.
Amesema taarifa walizozipokea kutoka nchi washirika, zinaenda sambamba na maelezo ya Uturuki ya tukio hilo.
"Ushirikiano tulioupata kutoka kwa washirika mbalimbali kwa leo unathibitisha taarifa tuliyoipata kutoka Uturuki."
Hata hivyo, Moscow bado wanasisitiza kwamba, ndege hiyo ilikuwa katika anga ya Syria, na kwamba hakukuwa na ukiukwaji wa anga ya Uturuki.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment