Wafugaji hao wenye zaidi ya ng'ombe elfu thelathini na wanne walioingia nao kutoka bonde la Ihefu mkoani Mbeya, wametoa ombi hilo katika kijiji cha Kidodoma.
Wamesema pamoja na kumpongeza Dakta JOHN MAGUFULI kwa kuchaguliwa kuwa rais wa serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wamemuombaawatambue wafugaji kwa sababu wanachangia pato taifa kupitia mifugo yao ingawa hawathaminiwi na mifugo yao inaonekana ni haramu.
Kwa upande wake, mwenyekiti wa kijiji cha Kidodoma Bwana ALIFA MAKUNGANYA amesema halmashauri hiyo ina uhusiano mazuri na wafugaji hao ambao wanachangia fedha katika maendeleo ya kijiji.


0 comments:
Post a Comment