Image
Image

Polisi nchini Kenya wamenasa noti bandia $693m.

Polisi nchini Kenya wamenasa noti bandia za jumla ya $693m (£485m) baada ya kufanya msako katika nyumba moja jijini Nairobi.
Watu wawili, mmoja kutoka Cameroon na mwingine kutoka Niger, wamekamatwa kuhusiana na pesa hizo.
Mkuu wa polisi Joseph Boinett akitangaza kupatikana kwa pesa hizo, amewaambia wanahabri kwamba hicho ni “kiasi kikubwa sana” cha pesa.
Amesema noti bandia za euro 369 milioni pia zimepatikana, pamoja na mitambo ya kutengeneza noti bandia.
Polisi walifanya msako baada ya kupokea habari za mfanyabiashara aliyetapeliwa Sh40 milioni za Kenya baada ya kuhadaiwa kwamba zingeongezwa mara tatu na kuwa Sh120 milioni.
Kwa jumla, pesa hizo zilizopatikana katika mtaa wa South C, zikibadilishwa na kuwa shilingi za Kenya zinafikia Sh110 bilioni ambazo ni sawa na shilingi trilioni 2.3 za Tanzania.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment