Image
Image

Kubwakuliko:Ray kutengeneza Documentary ya kunywa maji.

Muigizaji wa Bongo Movie nchini Tanzania Ray Kigosi amesema kuwa kutokana na mapokeo juu ya unywaji maji na kuwa mweupe anampango ambao anatarajia kutengeneza makala(Documentary)juu ya umuhimu wa maji.
Akizungumza wakati wa mahojiano yake na kituo kikubwa cha radio nchini Tanzania Ray amesema hayo na kusema kuwa baada ya suala hilo la unywaji maji na kuwa mweupe kuwa na kasi kila kona kwake yeye inamuongezea kitu flani kwani hata kampuni za uzalishaji maji zinaweza kumtumia.
Amesema ingekuwa nje ya Tanzania ingekuwa ni rahisi kwa aidia hiyo kuchukuliwa na hivyo kuangaliwa Product mbalimbali juu ya umuhimu wa maji kwa mwanadamu.
Hivi karibuni katika baadhi ya mitandao ya kijamii Ray amekuwa gumzo hadi sasa baada ya kuhojiwa kupitia Radio Clouds juu ya weupe wake na kusema kuwa kinachofanya hivyo ni kufanya mazoezi na kunywa maji kwa wingi,jambo ambalo limechukuliwa tofauti na jamii na kuona kuwa huenda kuwa hakuna ukweli juu ya hilo.
Badhi ya picha ambazo zimekuwa zikisambaa kupitia mitandao ya kijamii haswa kwenye mtandao wa Whatsapp zimekuwa zikionesha watu wakinywa maji kwa wingi kwa kutumia madumu makubwa na wengine kunywa visimani kama ng”ombe kusudi waone ninamna gani maji yanasaidia kubadilisha rangi ya mwili na kuwa mweupe.
Haya ni Mahojiano yanayokukumbusha alichokisema juu ya weupe wake kabla ya kuzua gumzo.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment