Image
Image

Van Gaal amewataka wachezaji wake kuwa na ''uchu'' katika mechi ya kombe la Europa

Mkufunzi wa kilabu ya Manchester United Louis Van Gaal amewataka wachezaji wake kuwa na ''uchu'' katika mechi ya kombe la Europa dhidi ya FC Midtylland.
United iko nyuma kwa mabao 2-1 na itaikaribisha timu hiyo ya Denmark nyumbani.
Na alipulizwa kile alichokihitaji kutoka kwa timu yake ,Van Gaal alijibu: Tamaa,njaa mara nyingi mimi hutumia neno ''uchu''.
Ufanisi katika ligi ya Europa ndio matumaini makubwa ya Manchester United kufuzu katika ligi ya vilabu bingwa Ulaya.
Baada ya kupoteza 2-1 kwa Sunderland katika ligi ya Uingereza,mashetani hao wekundu wana alama sita chini ya kilabu ya nne katika jedwali la ligi ya Uingereza.
Mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 64 anakabiliwa na madai kwamba huenda kazi yake ikachukuliwa na aliyekuwa mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho na amekuwa akikosolewa na mashabiki.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment