Image
Image

Washambuliaji wawili waliojilipua uwanja wa Ndege Brussels watambuliwa.

Washambuliaji wawili wa kujitoa mhanga waliojilipua katika uwanja wa ndege wa Brussels Jumanne wametambuliwa kuwa ndugu wawili, Khalid na Brahim el-Bakraoui.
Kituo cha runinga cha RTBF kimesema wawili hao walifahamika vyema na polisi.
Mwanamume wa tatu aliyeonekana kwenye video za kamera za siri uwanja wa ndege akiwa pamoja na wawili hao bado anasakwa.
Milipuko miwili ilitokea katika uwanja wa ndege na mwingine mmoja katika kituo cha treni na kuua watu 34 na kujeruhi wengine 250.
Ubelgiji imeanza siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

RTBF imesema ndugu hao wawili walifahamika na polisi na wana rekodi za uhalifu lakini hawakudhaniwa kuwa na uhusiano na ugaidi awali.
Kituo hicho cha runinga kimesema Khalid el-Bakraoui alitumia jina bandia kukodi nyumba katika eneo la Forest jijini Brussels ambapo polisi walimuua mtu mwenye silaha kwenye makabiliano wiki iliyopita.
Ilikuwa ni wakati wa msako huo ambapo polisi walipata alama za vidole za Salah Abdeslam, mshukiwa mkuu wa mashambulio ya Paris ya 13 Novemba.

Abdesalam alikamatwa kwenye operesheni ya maafisa wa usalama Ijumaa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment