Image
Image

Wasiwasi wa Kurudi ugonjwa wa EBOLA nchini Guinea watanda*Hivi karibuni uliuwa watu watano.

Ugonjwa wa EBOLA unaelekea kurudi kwa kasi nchini Guinea, kwani idadi ya watu waliokufa kutokana na mlipuko wa sasa wa ugonjwa wa EBOLA sasa imefikia watu watano.
Idadi hiyo imetolewa na maafisa wa afya waliokaririwa na mashirika ya habari na zaidi ya watu 800 ambao huenda waligusana na watu waliokufa wamewekwa chini ya karantini ya wiki tatu kufuatilia hali yao.
Kufuatia mlipuko huo wa sasa Lberia imefunga sehemu ya mpaka wake na Guinea.

Katika mlipuko wa kwanza mwaka 2013 zaidi ya watu 11,000 walikufa Guinea, Liberia na Sierra Leone na tangu mlipuko huo uthibitiwe nchi zote tatu zimeshuhudia milipuko mingine ya hapa na pale.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment