Image
Image

MACHAR hatimaye ameapishwa kuwa makamu wa rais wa kwanza nchini Sudan ya Kusini.

Aliyekuwa kiongozi wa waasi wa Sudan ya Kusini Bwana RIEK MACHAR hatimaye ameapishwa kuwa makamu wa rais wa kwanza nchini humo katika serikali mpya ya umoja.
Akizungumza baada ya kuapishwa amesem
a wakati umefika kuwaleta pamoja watu wa nchi hiyo ili waungane na kwamba ingawa kutakuwa na changamoto lakini moyo wa kisiasa utatua changamoto zote hizo kwa njia ya maridhiano.
Kwa upande wake Rais SALVA KIIR alisema amani ndiyo njia pekee ya nafuu kwa
wananchi wa Sudan ya Kusin
i kuondokana na mateso ya vita visivyostahili vilivyowakumba kwa zaidi ya miaka miwili.
Bwana KIIR amesema anaamini hiyo ndiyo njia pekee ya kurejea katika njia ya amani, utulivu na ustawi wa nchi hiyo ya Sudan ya Kuaini ambayo ni changa zaidi duniani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment