Image
Image

Bill Nas asalimu amri kwa Mzee kigogo - TID,afungukaa....

Msanii Bill Nas ambaye hivi karibuni amezua mzozo mkubwa na msanii TID ambaye amemsaidia kwa kiasi kikubwa kutoka kimuziki, amesema hapendezwi na kitendo cha kukosana naye kwani ni msanii ambaye anamuheshimu sana.
Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Bill Nas amesema TID ni mtu muhimu sana kwake kwani ana mchango mkubwa kwenye maisha yake na muziki wake kiujumla.
"TID ni mtu ambaye mi namuheshimu sana, ana mchango kwenye muziki wangu na mambo mengine, hata leo unaposikiliza ligi ndogo ni kati ya chorus kali sana ambazo mi naziheshimu sana, lakini kuhusu kutoka radar na vitu vingine, nilikuwa nataka nikutane naye mwenyewe kama mwanafamilia, kwa sababu naona ishu inaenda kwenye media", alisema Bill Nas.
Pia Bill Nas amesema hali hiyo inamuumiza hata kikazi pia, lakini ilimpasa kuondoka Radar, kwani muda wake wa kuwepo hapo ulishaisha.
"Kwa namna moja au nyingine hata mimi inanifrustrate sana kwa sababu kuna vitu vingi nataka kuvifanya, vitu vingi nataka kuviweka sawa, sasa ishu kama hii inaleta mkanganyiko fulani, lakini muda wangu mimi radar uliisha, natakiwa kufanya vitu vyangu vingine", alisema Bill Nas.
Hivi karibuni Bill Nas aliamua kuachana na Radar entertainment ambayo ipo chini ya TID, bila kutoa taarifa kwa msanii huyo, ambaye amechangia kwa kiasi kikubwa kufika alipo sasa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment