Image
Image

Durtete aapishwa kuwa rais wa 16 wa Ufilipino

Rais mpya wa Ufilipino Rodrigo Duterte ameapishwa leo, baada ya kuahidi kuwa vita kali dhidi ya uhalifu ndiyo kitakuwa kipaumbele cha mhula wake wa miaka sita. Durtete amekula kiapo mbele ya hadhira ndogo katika ikulu ya Malacanang, badala ya mkutano wa umma kama walivyofanya watangulizi wake. Programu yake ya kupambana dhidi ya uhalifu inahusisha mipango ya kurejesha adhabu ya kifo, amri za kupiga risasi na kuuwa kwa vikosi vya usalama na kutoa zawadi kwao kwa kuikabidhi miili ya wauzaji wa madawa ya kulevya. Akijibu hoja za wakosoaji wa mikakati yake ya kupambana na uhalifu na ufisadi, Duterte amesema: "Nataka niseme hivi: Nimeona namna rushwa ilivyoikosesha serikali fedha nyingi, zilizokuwa zimepangwa kwa ajili ya kuwaondoa mamilioni katika hali mbaya ya umaskini waliomo. Nimeona namna madawa haramu yanavyoharibu watu na kuvunja mahusiano ya kifamilia." Durtete, mwendesha mashtaka wa zamani mwenye umri wa miaka 71, na meya wa zamani wa mji wa kusini wa Davao, alipata ushindi mkubwa katika uchaguzi uliyofanyika mwezi Mei, na ameahidi kuwasafisha wahalifu nchini humo pamoja na wezi ndani ya serikali katika kipindi cha miezi sita.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment