Image
Image

Majaliwa aagiza kutumbuliwa kwa watakaobainika kutafuna fedha za CHF.

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza kufukuzwa kazi na kufikishwa mahakamani kwa watumishi wote wa Sekta ya Afya watakaobainika kula fedha zinazochangwa na wananchi kwa ajili ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). Pia amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Stephen na Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dk John Gurisha kusimamia na kulinda fedha za CHF zinazochangwa na wananchi na kuhakikisha zinatumika kama zilivyokusudiwa.
Alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara kwenye Jimbo la Kwela, Tarafa ya Mtowisa wilayani Sumbawanga.
“Kitendo cha kula fedha zinazochangwa na wananchi kwa lengo la kupata huduma za afya kinawafanya wakate tamaa ya kuendelea kuchangia mfuko huo. Kama wako watumishi wenye tabia hizo waache mara moja,” alisisitiza.
Mbali na kutoa agizo hilo kwa uongozi wa Mkoa wa Rukwa, pia Waziri Mkuu aliwataka wananchi kujiunga na CHF kwa sababu mfuko huo utawawezesha kupata huduma za matibabu bure wao na familia zao katika kipindi cha mwaka mzima.
Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema barabara ya kutoka Ntendo hadi Muze yenye urefu wa kilometa 85 itajengwa kwa kiwango cha lami ili iweze kupitika kwa urahisi na kuwawezesha wananchi kupata huduma kwa wakati.
Akizungumzia ombi lililotolewa na Mbunge wa Jimbo la Kwela, Ignas Malocha (CCM) la kutaka tarafa hiyo ya Mtowisa kuwa wilaya au halmashauri, Waziri Mkuu anakwenda kulifanyia kazi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment