Image
Image

Wananchi wa Gabon wanasubiri kutangaziwa matokeo ya uchaguzi wa urais.

Wananchi wa Gabon wanasubiri kutangaziwa matokeo ya uchaguzi wa urais, na wengi wana hofu ya kutokea kwa machafuko baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo leo Jumanne. Mshindi hajafahamika, licha ya kila upande kudai kushinda uchuguzi huo wa Jumamosi mwishoni mwa juma lililopita.
Rais anaye maliza muda wake, Ali Bongo Ondimba, anawania kinyanganyiro hiki kwa muhula wa pili wa mika saba, huku akishindana na Mwenyekiti wa zamani wa Tume ya Umoja wa Afrika, Jean Ping.
Waziri wa Mambo ya Ndani anatazamiwa kutangaza matokeo ya uchaguzi kuanzia saa 11 jioni saa za Gabon katika majengo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Cenap) wakati ambapo raia wa nchi hii wanaishi kwa hofu ya kutokea kwa machafuko tangu kufungwa kwa vituo vya kupigia kura Jumamosi jioni.
Kiongozi wa zamani wa chama cha majaji wakati wa utawala wa Omar Bongo Ondimba, na kiongozi wa upinzani baada ya uchaguzi wa mwanawe Ali Bongo mwaka 2009, Jean Ping, 73, anapania kuipindua familia ya Omar Bongo, madarakani tangu mwaka 1967 katika ukanda huo wa Afrika ya kati, ambapo kupishana katika madaraka si rahisi.
"Nimechaguliwa," alisema Jumapili Jean Ping, wakati ambapo rais anaye maliza muhula wake Ali Bongo anasubiri kutangzwa matokeo ya uchaguzi, akiwa na imani ya kushinda uchaguzi huo. Msemaji wake, hata hivyo alitangaza Jumamosi jioni kwamba Ali Bongo anaongoza kwa kura nyingi dhidi ya mpinzani wake, na hawezi kushindwa.
Utawala kwa upande wake umesema kuwa unaendelea kuimarisha usalama, huku kambi ya Jean Ping ikisema hautakubali kuibwa. Hofu ya kutokea kwa machafuko inaonekana baada kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi, kwani kila upande unadai kushinda uchaguzi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment