Image
Image

Dawa ya kwanza duniani ya kutibu ugonjwa wa kifua kuzinduliwa Kenya.

Dawa ya kwanza duniani ya kutibu ugonjwa wa kifua kikuu miongoni mwa watoto inatarajiwa kuzinduliwa leo siku ya Jumanne mjini Nairobi.
Hadi kufikia sasa,watoto hutumia dawa zinazotumiwa na watu wazima ambazo hugawanywa kusagwa na kutiwa katika maji.
Daktari Cherise Scott,mkurugenzi wa maswala ya magonjwa ya watoto katika muungano wa utengezaji wa dawa za TB ,anasema kuwa dawa hiyo mpya inaweza kuleta afueni kwa watoto milioni moja ambao huambukizwa kifua kikuu kila mwaka ,pamoja na waangalizi wao.
Kenya ndilo taifa la kwanza kutoa dawa hiyo mpya kwa raia wake huku mataifa zaidi yakitarajiwa kuendelea na utoaji wa dawa hizo katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Dawa hiyo ni mchanganyiko wa dawa tatu zinazotumiwa kutibu Tb,zikiwa zimechanganywa kikamilifu na kuwekwa ladha ili kuwavutia watoto.
Inaweza kuyayuka kwa urahisi ndani ya maji,hivyobasi kuifanya kuwa rahisi kutumia kila siku katika kipindi cha miezi sita.
Hadi kufikia sasa ,waangalizi wa watoto hulazimika kuzivunja dawa hizo kabla ya kuwapatia watoto hao.Dawa hizo ambazo ziko uchungu ni vigumu kumeza.
Ugonjwa wa kifua kikuu unaongoza miongoni mwa magonjwa hatari dunia,na huwaua watu 3000 kila siku.
Dawa hiyo mpya itayasaidia maisha ya watoto zaidi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment