Image
Image

Jaji ampinga Wakili kuzuia waandishi kortini jijini Dar es Salaam.

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imekataa maombi ya Wakili wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ya kuwazuia waandishi wa habari wasiandike kesi inayohusu utekelezaji wa amri iliyoitaka benki hiyo kulipa Sh bilioni 92.
Jaji Ama Munisi ametoa uamuzi huo baada ya Wakili wa Benki hiyo, Karim Rashid kudai kuwa kesi hiyo inasikilizwa faragha hivyo watu wengine wakiwemo waandishi hawaruhusiwi kusikiliza.
“Naona kuna watu wanaandikaandika humu ndani na wakati tunajitambulisha, hawajajitambulisha pia shauri hili linasikilizwa chamber (faragha) hapaswi mtu mwingine kusikiliza isipokuwa wahusika.” alisema Wakili Rashid.
Jaji Munisi amesema ingawa wanasikiliza kwenye chumba cha faragha, suala hilo lipo wazi na kesi hiyo si ya faragha, hivyo ni ruhusa mtu yeyote kuingia na kusikiliza.
Kesi hiyo ilitajwa leo kwa ajili ya kusikiliza pingamizi la Kampuni ya Coast Textiles Ltd kupinga maombi ya kusitisha utekelezaji wa amri ya kulipa fedha hizo yaliyowasilishwa na Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment