Image
Image

Upatikanaji wa dawa katika Bohari ya Dawa nchini (MSD) ni sawa na asilimia 53.

WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema hali halisi ya upatikanaji wa dawa katika Bohari ya Dawa nchini (MSD) ni sawa na asilimia 53, kwani kati ya dawa muhimu 135 zinazohitajika, zipo aina 71 ghalani. Pia alisema hali ya upatikanaji wa chanjo nchini utaimarika zaidi kuanzia Oktoba 2, mwaka huu baada ya kupokea shehena mpya.
Katibu mkuu wa wizara hiyo, Dk Mpoki Ulisubisya alisema juzi alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu taarifa iliyotolewa na taasisi isiyo ya kiserikali inayofuatilia masuala ya afya, Sikika kuwa MSD inakabiliwa na upungufu wa dawa na kutoa takwimu kuwa kuna makopo 173 tu ya dawa aina ya paracetamol nchini.
Dk Ulisubisya alisema hali ya upatikanaji wa dawa itaimarika zaidi Oktoba mwaka huu hasa kutokana na bohari ya dawa kutumia mikataba ya muda mrefu na washitiri ili kuimarisha upatikanaji wa dawa wa haraka, pindi zinapohitajika kulingana na fedha zilizopatikana.
Kwa mujibu wa Dk Ulisubisya, wizara kupitia MSD tayari imepokea makopo 10,000 ya vidonge vya paracetamol ambayo yameshasambazwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Pia mkataba kati ya MSD na mtengenezaji wa ndani wenye makopo mengine 138,000 ya vidonge vya paracetamol yenye ujazo wa vidonge 1,000 umekamilika, ambapo dawa hizo zinategemewa kuanza kupokewa kuanzia wiki ya kwanza ya mwezi wa Oktoba 2016.
Aidha dawa nyingine zilizokuwa zinahitajika zaidi ambazo ni antibiotics na dawa za kupunguza maumivu, ciprofloxacin, ceftriaxone, diclofenac, co-trimoxazole, amoxycyline, doxycycline na metronidazole ziliwasili makao makuu ya MSD, tayari zimeshapelekwa kwenye kanda zote za MSD tayari kwa kusambazwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Sako Mwakalobo amesema serikali imewalipa Sh bilioni 20 mpaka sasa, bado wanadai Sh bilioni 142.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment