Image
Image

Muigizaji MUHOGO MCHUNGU yu Buheri wa Afya,Uzushi unao enea hauna ukweli.

Mapema hivi leo Kumeibuka  taarifa za kuogofya jamii ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii nchini tanzania, hususani kwa njia ya Whatsapp na Instagram zikidai kwamba muigizaji mkongwe wa filamu Tanzania, Muhogo Mchungu amefariki dunia.
Taarifa hizi licha ya kuwa kwamba wasambaza uzushi huu hawajaanza kwa Muigizaji Muhogo mchungu wamekuwa wakisambaza mara kadhaa taarifa hizo hata kwa viongozi wakubvwa wa Serikali kuhusu jambo fulani lenye kushtua jamii.

Kwenye mitaa mbali mbali na Maofisini hivi leo wameshtushwa na Taarifa yenye kudai kuwa Muigizaji nguli Mzee Muhogo mchungu hatunaye ulimwenguni, huku waliowengi wakipatwa na bumbuazi ilikuwaje tena, nini kilimpata kitu ambacho kilikuwa na utata kwa kuwa hakuna aliyekuwa na taarifa kamili kuhusu hili.
Wakati nasi tukitaka kujua ukweli wa jambo hili kwamba je huenda ni kweli ama uzushi kutokana na msambaza taarifa za huyu kuzisambaza na hatimaye kufikia wengi kupitia mitandao ya kijamii, Baada ya muda kupitia mtandao wake wa Instagram, mwigizaji wa Bongomovie Batuli amekanusha taarifa hizo na kuandika maneno haya.

Batuli aliandika hivi…
”Muogopeni Mungu Nyie Mnaozusha Habari Za Vifo Kwa Watu Maarufu,, Mkumbuke Hakuna Atakayepaa Sote Njia Yetu Ni Moja, Tumieni Mitandao Vizuri Sio Sifa Wala Ujanja Kutengeneza Habari Zenye Uzushi Kila Baada Ya Muda Fulani, Kifo Ni Cha Wote Hakikimbiliki Mtambue Ipo Siku Na Nyie Mabingwa Wa Kuzusha Kitawatembelea Tu #MunguAnawaona#MolaAkupeMaishaMarefuBaba”

 Chonde chonde tujifunze kuandika taarifa zenye ukweli wa mambo kuliko kugushi taarifa zenye kuogofya jamii na familia, yafaa sheria ya mtandao ikaze kamba kwa wazushi wa taarifa ovu kwa taifa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment