Image
Image

Waziri mkuu wa zamani wa Israel Shimon Peres Afariki.

Waziri mkuu wa zamani wa Israel aliyewahi kuhudumu pia kama rais Shimon Peres amefariki dunia akiwa na miaka 93.
Aliugua kiharusi wiki mbili zilizopita na hali yake ikawa mbaya zaidi ghafla Jumanne.
Bw Peres, ambaye alikuwa mmoja wa waliosalia kutoka kwenye kizazi cha wanasiasa waliokuwepo wakati wa kuundwa kwa taifa la Israel mwaka 1948, alihudumu kama waziri mkuu wa nchi hiyo mara mbili na mara moja kama rais.
Alishinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka 1994 kwa mchango wake katika mashauriano yaliyopelekea kutiwa saini kwa mkataba wa amani kati ya Israel na Palestina mwaka mmoja awali.
Wakati mmoja, aliwahi kusema kwamba Wapalestina ndio "majirani wa karibu zaidi" wa Waisraeli na wanaweza kuwa "marafiki wa karibu zaidi".
Bw Peres amefariki akitibiwa katika hospitali moja iliyopo karibu na mji wa Tel Aviv mapema Jumatano, jamaa zake wa karibu wakiwa karibu naye.
Alikuwa amelazwa chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Sheba Medical Centre baada ya kupatwa na kiharusi 13 Septemba.
Rais wa Marekani Barack Obama amemweleza Bw Peres kama "rafiki wa karibu" kwenye taarifa, na akasema: "Aliongozwa na maono ya heshima na utu na alifahamu kwamba watu wenye nia njema wanaweza kustawi pamoja."
Bw Peres alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kwa pamoja na Waziri Mkuu Yitzhak Rabin, ambaye baadaye aliuawa, na Kiongozi wa Wapalestina Yasser Arafat.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment