Image
Image

Mfalme wa Morocco Mohammed VI yupo nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi.

Mfalme wa Morocco Mohammed VI yupo nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ambapo miongoin mwa mengine anatarajiwa kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais John Magufuli.
Mfalme Mohammed VI aliwasili Tanzania Jumapili akitokea nchini Rwanda.
Atafanya mazungumzo na Rais Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam, na baadaye wawili hao watashuhudia utiaji saini wa mikataba ya ushirikiano katika masuala ya kiuchumi na biashara kati ya Tanzania na Morocco.
Mfalme huyo ameandamana na ujumbe mkubwa wa wafanyabiashara.
Morocco inatafuta pia uungwaji mkono katika juhudi zake za kutaka kurejea katika Umoja wa Afrika (AU).


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment