Image
Image

Muuguzi kizimbani kwa kuiba mtoto wa kiume wa siku nne.

MUUGUZI wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, Scolastica Leoni (43) ambaye ni mkazi wa kata ya Sanawari amepandishwa kizimbani kujibu shitaka moja la kuiba mtoto mchanga wa kiume wa siku nne. Akisomewa mashitaka na Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Pennina Joackim mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha, Patricia Kisinda, ilidaiwa mshtakiwa alifanya kosa hilo Aprili 15, mwaka huu majira ya usiku wa manane akiwa kazini.
Mwendesha Mashitaka alidai kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo akiwa kazini katika Hospitali ya Mount Meru wakati akifahamu wazi kufanya hivyo ni kosa kisheria na ni kinyume cha sheria na kanuni na taratibu za kazi. Alidai muuguzi huyo akiwa mtumishi wa umma katika hospitali hiyo aliiba mtoto muda mfupi baada ya kuzaliwa.
Alidai mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume cha Kifungu 169 kifungu kidogo cha 1(a) cha Sheria na Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho 2002.
Mshtakiwa alikana shitaka na hakimu alisema dhamana ni haki ya mtu kwa mujibu wa sheria hivyo anatakiwa kudhaminiwa na wadhamini wawili wenye mali isiyohamishika yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 20.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment