Image
Image

Mwambusi:Kuondoka kwa Kocha Mkuu, Hans van Pluijm ni pigo.

KOCHA Msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi amesema wameumia kuondoka kwa Kocha Mkuu, Hans van Pluijm lakini hawana budi kusonga mbele na kuhakikisha wanaendeleza ushindi katika michezo iliyoko mbele yao ili kutetea taji lao la ubingwa wa Ligi Kuu Bara. Pluijm alijiuzulu kuifundisha Yanga juzi baada ya uongozi wa timu hiyo kufanya mazungumzo na Kocha mwingine kutoka Zambia, George Lwandamina ili kuchukua nafasi yake pasipo kumshirikisha. Kufuatia kujiuzulu huko, timu hiyo kwa sasa iko chini ya Mwambusi na wasaidizi wengine waliokuwemo tangu mwanzo hadi uongozi huo utakapoamua hatma yao.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi baada ya mchezo dhidi ya JKT Ruvu Mwambusi alisema walimzoea Pluijm kwani walifanya kazi vizuri na kwamba ushindi walioupata wa mabao 4-0 walitoa kama zawadi kwake ya kumuaga.
“Tulimzoea sana kwa sababu tulifanya naye kazi vizuri, ‘tutammis’ na niseme tu kwamba ushindi wa leo (juzi) tunampa zawadi kwake na kumtakia kila la heri huko aendako,” alisema.
Mwambusi alisema kuondoka kwa Pluijm hakutawafanya kurudi nyuma, tayari wamezungumza na wachezaji na kuangalia namna ya kuendelea na mapambano.
Akizungumzia mchezo dhidi ya JKT Ruvu Mwambusi alisema anashukuru kwa kupata matokeo kwani timu hiyo siku zote huwa ngumu.
Aliomba mashabiki wa Yanga kuendelea kuwaunga mkono ili kutimiza malengo waliyojiwekea. Kocha huyo wa zamani wa Mbeya City alisema wataendelea kujipanga kwa ajili ya mchezo ujao kuendelea kushinda. Ushindi wa Yanga umeendelea kuiweka timu hiyo katika nafasi ya pili ikijivunia pointi 24 katika mechi 11 ilizocheza.
Kwa upande wa Kocha wa JKT Ruvu, Malale Hamsini alisema timu yake ilikuwa na udhaifu kiasi cha kukubali kufungwa na kwamba wataendelea kurekebisha mapungufu yao kufanya vizuri.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment