Image
Image

Rais Magufuli amteua Diwani Athuman kuwa RAS Kagera na Jaji Warioba awa mkuu wa chuo SUA.

                             DIWANI ATHUMAN - Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera.
Rais Dakta JOHN POMBE MAGUFULI leo amemteua aliyekuwa Mkurugenzi wa Up elelezi wa Makosa ya Jinai - DCI-   . DIWANI ATHUMAN kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera.
Uteuzi  huo  wa DIWANI ATHUMAN unaanza mara moja.
Rais MAGUFULI   pia  amemteua Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,  Jaji JOSEPH SINDE WARIOBA kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo -SUA, uteuzi huo umeanza juzi.
Wakati huo huo, Rais MAGUFULI amefanya uteuzi wa Wenyeviti wa Bodi katika taasisi tano za Serikali  ambapo Dakta JONES   KILIMBE kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlak a ya Mawasiliano Tanzania -TCRA- na amemteua SYLVESTER MABUMBA kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlak a ya Mawasiliano Tanzania, uteuzi ulioanza jana .
Rais MAGUFULI pia  amemteua Prof esa  PATRICK MAKUNGU kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo  ambao umeanza jana.
Uteuzi mwingine ni wa  MARTIN MADEKWE kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Fidia ya Ardhi  ulioanza jana na Rais  MAGUFULI pia amemteua  Prof esa  RAPHAEL TIHELWA CHIBUNDA kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wakurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Viu atilifu vya Kitropiki Tanzania -TPRI- Uteuzi  ulioanza hapo jana.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment