Image
Image

Serikali:Tutahakikisha mashindano ya ulimbwende yanakuwa na thamani na yenye faida.

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha mashindano ya ulimbwende yanakuwa na thamani na yenye faida. Nape aliyasema hayo wakati akimkabidhi bendera ya Taifa, Miss Ilala 2016, Julitha Kabete ambaye pia ni mshiriki wa mashindano ya Miss Tanzania 2016, ambaye anakwenda kushiriki mashindano ya urembo Afrika yatakayofanyika Novemba 26 katika kitongoji cha Calabar nchini Nigeria.
“Tunataka mashindano ya Miss Tanzania ambaye anafaidika sio mshindi peke yake tumeona hapa huyu alikuwa mshindi wa nne na amepata nafasi ya kuwakilisha nchi, tunafahamu mashindano ya Miss Tanzania yalikuwa yamefungiwa kufanyika ila sasa yamerudi vizuri, tutaendelea kuyaimarisha yawe bora na matarajio ya serikali ni kuona tunakuwa tunafanya vizuri na siku moja hata mshindi wa Miss World atoke Tanzania,” alisema Nape.
Pia Nape alisema serikali inamtakia safari njema na ipo nyuma yake kumpa msaada pindi unapohitajika.
Akizungumza wakati wa kukabidhiwa Miss Julitha Kabete amesema amejiandaa kwa ajili ya mashindano hayo na anaamini atafanya vizuri kwenye mashindano hayo ambayo ndio kwanza yanaanza.
“Naomba Watanzania wanisapoti ili nifanikiwe kushinda Miss Africa ambayo inafanyika Nigeria, ni nafasi ya kipekee ambayo nimepata na nikipata ushindi ni wetu sote,” alisema Julitha.
Mashindano hayo yatafanyika kwa mara ya kwanza Afrika katika kitongoji cha Calabar kilichopo Nigeria. Naye mrembo huyo akizungumza katika hafla hiyo alisema kuwa amejiandaa vizuri kwa ajili ya shindano hilo la kwanza kufanyika.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment