Image
Image

Upelelezi dhidi ya 'SCOPIONI' Ngoma nzito.

Dar es Salaam.Upande w Jamhuri kwenye kesi ya Salim Njwete anayetuhumiwa kumwibia Saidi Mrisho na kumtoboa macho kwa kisu umedai mahakamani hapo kuwa upelelezi haujakamilika na kuomba siku nyingine ya kukamilisha.
Mshitakiwa Njwete mwenye (34) ambaye ameshitakiwa kwa kumuibia Mrisho na kumjeruhi kwa kumchoma tumboni, mabegani na Machoni.
Taarifa ya Upelelezi kutokamilika ilielezwa na jana na Mwendesha Mashitaka Chensensi Gavyole mbele ya hakimu Mkazi Flora Haule kesi hiyo iliyotajwa na kuangaliwa kama upelelezi umekamilika.
       "Mshitakiwa yupo mbele ya Mahakama hii lakini upelelezi bado haujakamilika, tunaomba Mahakama itupangie siku nyingine ya kutajwa kutokana na upelelezi kuendelea" alisema Gavyole.
   Kutokana na sababu hizo, Hakimu Haule aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 16 itakapo tajwa tena.
Mshitakiwa huyo maarufu kama Scopioni alifikishwa Mahakamani hapo akiwa kwenye gari dogo la mizigo tofauti na siku za nyuma ambapo alikuwa akiletwa akiwa kwenye basi la Magereza.
Awali alidaiwa kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Septemba 9 Buguruni Sheli alipomuibia Mrisho fedha na vitu vyenye thamani ya Sh.476,000 na kumjeruhi kwa kumchoma kisu tumboni, mabegani na machoni. 
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment