Image
Image

Mbowe alipuwa bomu la wabunge wa CCM kupewa Milioni 10 kupitisha Muswada wa Habari bila kupingwa.

Leo 03/11/2016, bungeni Naibu spika amekataa katakata Waziri mkuu kujibu swali la Mbowe kwa waziri mkuu kuhusu tuhuma za wabunge wa CCM kuitwa kwenye kikao na kupewa fedha kiasi cha milioni 10 kila mmoja ili wasiibane serikali kwenye muswada wa sheria unaowasilishwa kesho.
Maelezo ya Naibu spika ni kuwa swali hilo halihusu sera, huku Mbowe akidai linahusu sera kwa kuwa ni rushwa kwa wabunge.
Baada ya Naibu Spika kukataa waziri Mkuu kujibu swali la Mbowe zikaendelea kusikika sauti za chini chini za wabunge, wengine wakisema acha ajibu usimzuie, huku minong'ono ya kila aina ikisikika kuhusu tuhuma hizo.
Kufuatia hatua hiyo katika baadhi ya Maeneo nchini Tanzania, imezuka minong'ono kuwa kwanini Naibu Spika asinge weza kuruhusu waziri mkuu kujibu swali hilo kama maswali mengine huku ikionekana sintofahamu kwamba pengine kuna ukweli juu ya hilo ama la.
Hii ni video ambayo Mbowe aliuliza swali hilo.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment