Image
Image

Uingereza muda wowote kuanzia sasa kujiondoa EU.

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ametia saini barua ambayo itaanzisha rasmi mchakato wa kuiondoa Uingereza kutoka kwa Muungano wa Ulaya.
Barua hiyo inatoa taarifa rasmi ya kujiondoa kwa muungano huo kwa kitumia Kifungu 50 cha Mkataba wa Lisbon.
Itawasilishwa kwa rais wa Baraza la Ulaya Donald Tusk baadaye leo.
Kwenye taarifa kwa bunge la chini nchini Uingereza, Bi May baadaye anatarajiwa kuwaambia wabunge kwamba hatua hiyo inaashiria "wakati we taifa letu kuungana pamoja."
Hatua hiyo imechukuliwa kutokana na kura ya maoni iliyoandaliwa Juni mwaka jana, ambapo wapiga kura waliunga mkono kujiondoa kutoka kwa EU.
Barua ya Bi May itawasilishwa kwa Bw Tusk Jumatano mwenzo wa saa sita unusu adhuhuri saa za Uingereza na balozi wa nchi hiyo katika EU Sir Tim Barrow.
Waziri mkuu ambaye ataongoza kikao cha baraza la mawaziri asubuhi, baadaye atatoa hotuba rasmi kwa wabunge kuthibitisha kwamba mchakato wa Uingereza kujiondoa EU umeanza.
Ataahidi "kuwakilisha kila mtu katika Uingereza yote" wakati wa mazungumzo hayo - wakiwemo raia wa EU (wanaoishi Uingereza), ambao bado haijafikiwa uamuzi kuhusu hatima yao baada ya Uingereza kujiondoa kutoka kwa muungano huo.
"Nimejitolea kuhakikisha tunapata mkataba bora zaidi kwa kila mtu katika nchi hii," anatarajiwa kusema.
"Kwani, tunapokabili fursa na changamoto zilizopo mbele yetu, maadili yetu ya pamoja, maslahi na ndoto zetu zinaweza - na ni lazima - zitulete pamoja."
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment