Image
Image

Guterres ikosoa Marekani kuondoa mfuko wa fedha wa kusaidia afya ya uzazi wa mpango duniani

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa amekosoa uamuzi wa Marekani wa kuondoa fungu la pesa kutoka kwenye mfuko wa umoja wa mataifa unaoshughulikia idadi ya watu uliokuwa ukisaidia masuala ya afya ya uzazi na uzazi wa mpango duniani.
Antonio Guterres amesema kupoteza pesa hizo takriban dola milioni thelathini na mbili mwaka huu pekee, kunaweza kuleta madhara makubwa kwa afya za wanawake na watoto wanaohitaji msaada.
Wizara ya mambo ya nje imesema inasitisha uchangiaji kwenye mfuko huo kwa sababu shirika hio linaunga mkono programu ya china ya utoaji mimba.
Taasisi hiyo ya umoja wa mataifa imesema haiungi mkono wala kusaidia vitendo vya utoaji mimba, pia haijavunja sheria yeyote ya Marekani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment