Image
Image

Tiger Woods kurejea tena katika mchezo wa gofu.

Tiger Woods anatarajiwa kurejea tena katika mchezo wa gofu miezi nane baada ya kuandamwa na majeraha.
Atajitupa uwanjani kuanzia Novemba 30 mpaka Desemba 3.
Woods mshindi wa vikombe 14 vya kimataifa, anapona majeraha ya upasuaji wa mgongo aliyofanyiwa miaka mitatu iliyopita ambayo kwa wakati fulani alikuwa akirudia upasuaji mara kwa mara na kumfanya kuwa dhaifu.
Alijiondoa katika michuano ya Dubai mwezi Februari kwa sababu hiyohiyo.
''Ninajipanga kurejesha heshima yangu, furaha yangu na uwezo wangu kupitia mchezo ninaoupenda, alisema Woods''
Woods hajashinda taji lolote kubwa tokea mwaka 2008.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment