Image
Image

Kigwangalla amsimamisha kazi Mkurugenzi wa wanyamapori Serengeti.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dr. Hamis Kigwangalla amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa wanyamapori wa hifadhi ya Serengeti, kwa tuhuma mbalimbali zinazomkabili.
Akizungumza ndani ya Hifadhi ya Serengeti, ambapo amefanya ziara ya kushtukiza , Dr. Kigwangalla ameagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Wanyama Pori, Prof. Alexander Songorwa mara moja
Tuhuma hizo zimetajwa kuwa ni kuhujumu Serikali kwa kutoa taarifa za siri za Serikali kwa vyombo vya habari na kutunga taarifa zenye kulenga kuchochea mgogoro wa Loliondo.
“ Juzi usiku zilizunguka taarifa kwamba Dkt. Kigwangalla yupo na msafara wa gari mbili binafsi (private) njiani kwenda Loliondo na kwamba atalala Hotel ya Acacia iliyopo Karatu. Leo msafara wangu umekuwa ukifuatiliwa na watu wasiojulikana ambapo kila hatua aliyofikia ilikuwa ikiripotiwa kwenye mtandao”. Amesema Kigwangalla katika taarifa hiyo
Aidha Prof. Songorwa amekuwa akihusishwa na kashfa ya kushiriki kugawa vitalu vya uwindaji kinyume cha sheria pamoja na tuhuma nyingine.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment