Image
Image

EXCLUSIVE: LHRC YAMTAKA WAZIRI MKUU PINDA KUFUTA KAULI YAKE ALIYOITOA BUNGENI JUNE 20 MWAKA HUU.


Kituo cha sheria na haki za binadamu - LHRC kimesema kinaendesha mchakato wa kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali na kisha kuandaa waraka kupinga kauli ya waziri Mkuu Mizengo Pinda bungeni ambayo kituo hicho kinadai imebariki vyombo vya ulinzi na usalama hususan jeshi la polisi kuwapiga wananchi watakaokaidi na kupinga amri halali ya jeshi hilo.

LHRC na baadhi ya wadau hao wanamtaka waziri mkuu Mizengo Pinda kufuta kauli yake hiyo sambamba na kulielekeza jeshi la polisi kufanya kazi kwa mujibu wa  sheria na taratibu zilizoko katika kutekeleza majukumu yake ya  kulinda usalama wa raia na mali zake.
Mizengo Pinda - waziri mkuu Tanzania
Kauli hiyo imekuja muda mfupi wakati akizungumza na  waandishi wa habari, jijini Dar es salaam, Ambapo  Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Dk Hellen Kijo Bisimba, amedai kuwa kwa sasa maudhui ya kauli hiyo ni kinyume na cha katiba, sheria za nchi na misingi ya haki za binadamu hasa katika kipindi hiki ambacho kumekuwa na matukio mengi ya ukiukwaji wa haki za binadamu yanayodaiwa kuhusisha na vyombo vya dola.
Dk Hellen Kijo Bisimba - Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC

Juni 20 2013 katika kipindi cha maswali na majibu Bungeni mjini Dodoma, katika mkutano wa 11 kikao cha 53 cha Bunge la Bajeti, Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akijibu swali la Mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa na serikali kufuatia kuwepo kwa matukio ya vurugu za mara kwa mara Waziri Mkuu pamoja na mambo mengine alikaririwa kusema vyombo vya ulinzi na usalama vitalazimika kuchukua hatua kali ikiwemo kuwapiga wananchi wanaokaidi amri halali ya jeshi hilo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment