Rais wa shirikisho la mpira
wa miguu nchini Tanzania (TFF) Leordger chila Tenga ametangaza kikosi cha Taifa
stars chenye uwezo wa kuweza kukabiliana na mikiki mikiki katika mashindano
yoyote yale kutokana na uimara wake.
Mapema leo Tenga wakati akizungumza na wachezaji wa timu
ya stars kwenye Hotel ya Tansoma jijini
dar es salaam amesema kuwa kiwango walicho onyesha wachezaji hao kwenye mechi
zilizokuwa zimepita za mchujo kama ya
Morocco na Ivory imethibitisha tosha
kiwango cha timu hiyo.
"Kiwango mlichoonyesha
katika mechi hizo kila mtanzania anayewafuatilia amekiona, hivyo hatuna shaka
kuwa mtatuwakilisha vizuri kwenye mechi ya kesho dhidi ya uganda," amesema
rais tenga na kuwataka kupigana kwa ajili ya tanzania.
Tenga amesema TFF,
mdhamini kilimanjaro premium lager, kamati ya ushindi na watanzania kwa ujumla
wanawaunga mkono kwani wamekuwa wakiboresha kiwango chao kila wanavyozidi
kucheza mechi tangu wake chini ya kocha kim poulsen, mei mwaka jana.
Taifa stars inayodhaminiwa na
kilimanjaro premium lager kesho (julai 13 mwaka huu) saa 9 kamili alasiri
uwanja wa taifa, dar es salaam itacheza na uganda (the cranes) katika mechi ya
kwanza ya raundi ya mwisho kuwania tiketi ya kucheza fainali za chan zitakazofanyika
mwakani nchini afrika kusini.
Wakati huo huo, tenga
ameahidi kumpatia tiketi ya kwenda uganda kwenye mechi ya marudiano mshabiki
wiseman mwakyusa luvanda anayetembea kwa miguu kutoka mbeya kuja dar es salaam
kushuhudia mechi ya kesho.
"Kama ni kweli anakuja
kwa kutembea, huyu ameonyesha kiwango kikubwa cha uzalendo kwa timu ya taifa,
nitampatia tiketi ya kwenda kampala kuishangilia taifa stars kwenye mechi ya
marudiano," amesema rais tenga.
Katika hatua nyimngine makocha
wa timu hizo kim poulsen wa taifa stars na sredojvic micho wa the cranes
wamesema mechi ya kesho itakuwa ngumu kwa vile kila mmoja amejiandaa
kuhakikisha anafanya vizuri.
Wakizungumza na waandishi wa
habari leo, makocha wote waliezea ubora wa wapinzani wao, lakini wakasisitiza
kuwa wanaingia uwanjani kuhakikisha wanashinda ili kujiweka katika mazingira
mazuri kwa ajili ya mechi ya marudiano itakayochezwa kampala wiki mbili zijazo.
kim alisema uganda ndiyo
inayoongoza kwa ubora wa viwango vya fifa katika ukanda huu wa afrika mashariki
na kati, hivyo ni changamoto kwao ingawa wachezaji wake tayari wamejipanga
vizuri kwa ajili ya mechi hiyo.
Kwa upande wake micho aliyefuatana na
nahodha wake hassan wasswa alisema taifa stars imekuwa ikifanya vizuri tangu
iwe chini ya kim, na itakuwa na wachezaji tisa wa kikosi cha kwanza
kinachocheza mechi za mchujo za kombe la dunia wakati kwa upande wake atakuwa
na wachezaji wawili.
0 comments:
Post a Comment