Image
Image

JICA LAIKABIDHI TANESCO KITUO CHA KUPOZEA UMEME WILAYA YA ILALA JIJINI DAR ES SALAAM



Mkurugenzi wa Tanesco, Felchesmi Mramba (wa tatu kushoto)  sambamba na  mwakilishi wa shirika la kimataifa la JICA, Yasunori Onishi.jijini Dar es Salaam.

Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (Jica) limelikabidhi Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), kituo cha kupozea umeme kilichopo wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam baada ya kukifanyiwa ukarabati uliogharimu Dola za Marekani 500,000.

Makabidhiano hayo yaliyokwenda sambamba na kutiliana saini yalifanyika  jijini Dar es Salaam baina ya Kaimu Mkugenzi wa Tanesco, Felchesm Mramba na Mwakilishi wa Jica, Yasonari Orishi ambaye aliongozana na ujumbe wa shirika hilo kutoka Japan.

Mramba alisema kukabidhiwa kwa kituo hicho ni hatua nzuri kwani  inaimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika jijini Dar es Salaam na kwamba Jica wamefunga mitambo ya kisasa inayotumia gesi.

 Ukarabati wuliofanywa katika kituo hicho ni utekelezaji wa mipango ya uboreshaji wa upatikanaji wa umeme na kwamba kuna vituo vingine vipya vinavyotarajia kujengwa eneo la Kurasini, Mbagala, Gongolamboto na Kinyelezi.

Aliongeza kwa kusema kuwa vipo vituo vingine 18 vinavyojengwa na kukarabatiwa katika jiji la Dar es Salaam na kuwataka wakazi wa jiji hilo kuwa wavumilivu kwani tatizo la upatikanaji wa umeme ufumbuzi wake utapatikana hivi karibuni.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment